Jenerali Francis Ogolla atazikwa Jumapili tarehe 21

  • | Citizen TV
    1,001 views

    Jenerali Francis Ogolla atazikwa jumapili tarehe 21 nyumbani kwake. Kwa mujibu wa familia yake, Ogolla alikuwa ameacha wosia na kusema kuwa angependa mazishi yake yafanyike saa 72 baada ya kifo chake. Familia yake imesema kuwa Ogolla atazikwa kulindana na azma yake nyumbani kwake katika kijiji cha Mor, huko Alego, kaunti ya Siaya. Ibada fupi ya wafu ya kumwomboleza jenerali ogolla itafanyika katika kanisa alilokuwa akihudhuria la Nduru kabla ya mazishi. Baadaye ibada nyingine ya kumkumbuka itafanyika Ijumaa tarehe 26 katika uga wa ulinzi sports complex ambako alikuwa akifanyia mazoezi kila wiki.